Watson,Edmund watinga raundi ya pili

Wacheza tenesi Heather Watson na Kyle Edmund wamefuzu kuingia raundi ya pili ya michuano ya wazi ya ufaransa.Watson, alimshinda mpinzani wake Nicole Gibbs, kwa seti mbili baada ya kupoteza seti ya kwanza kwa 5-7 kisha akashinda kwa 6-2 6-2.
Gibbs alikua anaongoza katika mchezo wa kwanza uliofanyika siku ya jumapili ambao haukuweza kumalizika kutokana na mvua kali kunyesha uwanjani na huu ni ushindi wa tano mfululizo kwa Watson.
Nae Kyle Edmund akaibuka kidedea kwa kumchapa Nikoloz Basilashvili kwa seti tatu kwa ushindi wa 7-6 kisha akapoteza kwa 6-7 na kumaliza na ushindi wa 7-5 6-1.
Previous
Next Post »