Afrika Kusini yaadhimisha maandamano dhidi ya ubaguzi wa rangi

Afrika Kusini inaadhimisha miaka 40 tangu maandamano ya wanafunzi wa Soweto, walipopinga ubaguzi wa rangi katika elimu kwa kulazimishwa kusomeshwa kwa lugha ya Ki-Afrikaan.
Mamia ya wanafunzi walifariki katika vurugu zilizojiri wakati serikali ya ukoloni ya wazungu makaburu ilipotumia nguvu kupita kiasi, kujaribu kuzima maandamano hayo.
Maandamano hayo yalikuwa kama mwanzo wa kuelekea hatua za kumalizwa kwa utawala wa makaburu wa Afrika Kusini.
Makamu wa rais wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa, ameweka shada la maua kwenye kaburi la kijana Hector Pietersen.

Image caption


Ni picha ya mwili wa kijana huyo uliokuwa unabebwa na mwanafunzi mwenzake baada ya kupigwa risasi na polisi.
Picha hiyo ilibua hamasa na hasira kubwa na kuufanya ulimwengu kulaani ukatili uliokuwa ukiendelezwa na utawala wa ubaguzi wa rangi nchini humo.
Previous
Next Post »