ONDOA VINYWELEO USONI KWA KUTUMIA BINZARI MANJANO.


Yes ladies kila mmoja wetu anavinyweleo usoni, but sema tu kwa wengine huonekana more kuliko wengine..na kama bado hujapata solution ya kuondoa basi leo ndio nimewaletea..Nadhani utakuwa umenotice kuwa ukipaka makeup au hata powder tu inakuwa inakaa kwa juu ya vinyweleo na huleta muonekano mbaya, basi fuata hii process fupi tu kuweza kuondoa vinyweleo usoni.
Chukua vijiko 2 vikubwa vya binzari manjano, changanya na maji ya uvuguvugu kidogo upate mchanganyiko mzito.

Paka katika sehemu ambayo unataka vinyweleo hivyo kuondoka kabisa, then acha ikae kwa dakika 20-30.

Chukua kitambaa na maji ya baridi kisha lowesha kitambaa na uanza kusugua hiyo sehemu uliyopaka mchanganyiko wako wa binzari manjano.
Fanya hivi kila siku, na siku sinavyozidi kwenda utaona vinyweleo vinapungua na hatimaye kuisha kabisa. Hii itafanya iwe vigumu kwa vinyweleo kuota usoni.

Previous
Next Post »