MAREKANI YASIKITISHWA NA VITENDO VYA UKATILI NA UTEKAJI NCHINI TANZANIA

Ubalozi wa Marekani Tanzania unataka uchunguzi huru kuhusu matukio ya matumuizi ya nguvu dhidi ya harakati za kisiasa za upinzani.
Hii ni baada ya kifo cha mjumbe wa chama cha upinzani CHADEMA, Daniel John tarehe 11 Februari, ambaye mwili wake ulipatikana katika fukwe za bahari ya hindi, jijini Dar es salaam, siku moja baada ya kutekwa ukiwa na majeraha ikiwemo shingo yake kunyongwa na watu ambao hadi saa hawajajulikana.
Marehemu anaripotiwa kutekwa pamoja na mwenzake, Reginald Mallya aliyenusurika na kupatikana akiwa hai akiwa na majeraha kadhaa sehemu za mkononi na kichwani.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwenye mtandao wa balozi wa Marekani, balozi wamesema "Tunatuma salamu zetu za rambirambi kwa familia na marafiki wa marehemu kwa msiba huu."
"Kuongezeka kwa makabiliano ya kihasama na vitendo vya kikatili ni jambo linalotutia wasiwasi na kutusikitisha sana."
Pamoja na hayo ubalozi umetaka "uchunguzi wenye uwazi ili kuwawajibisha wale wote wanaohusika na vitendo hivi vya kikatili kwa mujibu wa sheria za Tanzania."
Tukio hilo limefayika ikiwa ni juma la mwisho la kampeni za uchaguzi mdogo katika majimbo mawili nchini Tanzania ambayo yalipoteza wabunge wake kwa sababu mbalimbali ikiwemo ile ya wabunge wa upinzani kujiuzulu kwa kile walichokiita kuunga mkono jitihada za Rais Magufuli na serikali ya awamu ya tano.
Kwa upande wake, kamanda wa polisi wa mkoa wa kipolisi wa Kinondoni, Jumanne Murilo, amesema polisi waachwe wafanye uchunguzi kufuatia vitendo hivyo vya utekaji nyara.
Haki miliki ya pic
Kumekuwa na kinachoonekana kama muendelezo wa vitendo vya mashambulizi dhidi ya wanachama wa upinzani,hivi karibuni nchini Tanzania. Kikubwa kikiwa ni shambulio dhidi mnadhimu mkuu wa chama cha upinzani nchini Tanzania Chadema, Bw Tundu Lissu anayezidi kupata matibabu nchini Ubelgiji baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana jijini Dodoma mwaka uliopita.
Previous
Next Post »