JE WAJUA TB INATIBIKA ENDAPO UKIWAHI MATIBABU


Karibu mpenzi  msomaji katika  makala ya afya yako na hapa tunaangazia magonjwa mbali mbali na kukumbushana pale tuliko jisahau kuhusu afya zetu  leo tutaongelea  ugonjwa wa kifua kikuu ambao ni tishio kubwa

 Kifua kikuu (kwa Kiingereza tuberculosis, kifupi TB) ni ugonjwa wa kuambukizwa ulio hatari. Ugonjwa huu husababishwa na aina mbalimbali za bakteria ambazo hujulikana kama Mycobacterium tuberculosis.

Kifua kikuu kwa kawaida kinaathiri mapafu, lakini pia kinaweza kuathiri sehemu nyingine za mwili.

Kifua kikuu husambazwa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine kwa kupitia hewa wakati anapokohoa, kupiga chafya, aumate yake yakiwa hewani

Maambukizi mengi hayana dalili wala hayaleti madhara. Lakini moja kati ya maambukizo kumi yasiyoleta madhara hatimaye huendelea na kuwa ugonjwa kamili. Kama kifua kikuu kisipotibiwa, kinaua zaidi ya 50% ya watu walioambukizwa.

Dalili za kifua kikukuu ni pamoja na kukohoa kwa wiki mara mbili au mfululizo homa za mara kwa mara kwa wiki mbili au zaidi,kutokwa kwa jasho jingi hasa kwa nyakati za usiku,kukohoa makohozi yenye damu, kupungua uzito zaidi ya kilo 3 ndani ya wiki 4 au kukonda na kukosa hamu ya kula


Maambukizi ya viungo vingine husababisha dalili mbalimbali. Njia ya kitaalamu ya utambuzi wa kifua kikuu kwa kutumia eksirei ya kuchunguza ugonjwa hujulikana kama eksirei ya kifua na pia wanatumiahadubini na kufanya uchunguzi wa vimelea maradhi vya majimaji ya mwilini. Uchunguzi wa kifua kikuu kisicholeta madhara hutumia kipimo kiitwacho kipimo cha ngozi (TST) na vipimo vya damupamoja na Kifua kikuu hugundulika kwa kupima makohozi na ikibidi x-ray na matibabu yake  ni bure katika hospitali zote za serikali na binafsi

Unapoona mtu ana dalili moja wapo kati ya hizi au wewe mwenyewe mshauri awahi kituo cha huduma za afya kwa uchunguzi tiba na awasiliane na mratibu  wa kifua kikuu aliye karibu nae kwani mmoja huweza kuambukiza watu kati ya 10 hadi 15 kwa mwaka kamam ajapata matibabu.wastani  wa watu  176 huugua kifua  kikuu kila siku nchini Tanzania na wastani  wa watu 12hufariki dunia kila siku

Ikitokea umegundulika kua unakifua kikuu usihofu kwani kinatibika na mamilioni ya watu duniani kote wameugua na kupona. Unachotakiwa kufanya ni kufatisha masharti utakayopewa na daktari kama; kunya dawa kila siku kwa muda uliopangiwa ili kupona kabisa. Matibabu yake huchukua huchukua kati ya miezi sita hadi minane



Endapoumegundulika na kifua ki kuu kumbuka kufunika mdomo na pua unapo kohoa au kupiga chafya ili usiambukize watu wengine na pia usiteme mate ovyo

Pumzika kiasi cha kutosha,kula chakula chakula bora na uwafahamishe ndugu  na marafiki kwamba unaugua kifua kikuu na uko kwenye matibabu na ukisha kamilisha matibabu nenda kwa uchunguzi ili kutibitisha  kama umepona.

Kumbuka ni muhimu kuendelea kutumia dawa mpaka mwisho hata kama unajisikia vizuri ili usipate kifua kikuu sugu ambacho matibabu yake ni magumu. Mara kwa mara kifua kikuu kimekuwa kikihusishwa na na ugonjwa wa ukimwi kwani asilimia 50 ya watu wenye kifua kikuu wana  VVU kama umethibitika unakifua kikuu ni muhimu ukapata ushauri na saa na kupima virusi vya ukimwi,kwani asilimia 10-15 ya watu wanao ishi na VVU waugua  kifua kikuu hivyo ni muhimu kuchunguzwa  kama una kifua kikuu ili kuboresha na kuokoa maisha yako kwani kifua kikuu kinatibika kabisa hata kama unamaambukizi ya VVU



Na pia ili kuzuia kifua kikuu, ni lazima watu wapimwe ugonjwa na wapate chanjo ya bacillus Calmette - Guérin.

Wataalamu wanaamini kwamba theluthi moja ya idadi ya watu duniani waliambukizwa kifua kikuu, na kila sekundekuna mtu ambaye anaambukizwa Mwaka 2007, kadri ya watu 13,700,000 duniani waliambukizwa kifua kikuu kinacholeta madhara sugu  Mwaka 2010, kadri ya milioni 8.8 ya watu waliambukizwa na milioni 1.5 ya watu walifariki baada ya kuambukizwa na kifua kikuu, na wagonjwa wengi wanapatikana katika nchi zinazoendelea  Idadi halisi ya wagonjwa wa kifua kikuu imekuwa ikipungua tangu mwaka 2006, na kesi mpya zimeshuka tangu mwaka 2002



Kifua kikuu si ugonjwa unaosambazwa sawasawa duniani kote. Kadri ya 80% ya watu katika nchi nyingi za Asia na Afrika waliofanyiwa kipimo cha ngozi walionekana wameambukizwa, lakini ni asilimia 5-10% tu ya wananchi wa Marekani ambao walionekana na ugonjwa huo. Watu wengi waliopo katika nchi zilizoendelea  wanaambukizwa kifua kikuu kwa sababu ya kutokuwa na kinga. Kwa kawaida, hawa watu wanaambukizwa kifua kikuu baada ya kuambukizwa na VVU na hatimaye wanapatwa na UKIMWI.

  TIBA

Kwa kawaida, mgonjwa wa kifua kikuu anatumia vidonge kila siku wakati wa matibabu yanayosimamiwa.

Ugonjwa wa kifua kikuu kikali unaweza kutibiwa kwa mchanganyiko wa antibiotics. Mchanganyiko sahihi wa dawa za kifua kikuu hutoa kinga na tiba.

Tiba inayofaa humwezesha haraka mgonjwa wa kifua kikuu kutoambukiza na kwa hiyo huzuia kuenea zaidi kwa kifua kikuu. Kufanikisha tiba ya TB, huchukua miezi sita hadi minane ya matumizi ya dawa ya kila siku.

Dawa za aina mbalimbali zinatakiwa kutibu kifua kikuu kikali. Kutumia dawa mbalimbali kufanya kazi nzuri ya kuua bakteria wote na huenda ikakinga dhidi ya usugu kwa dawa.

Dawa zinazotumika zaidi ni Isoniazid, Rifampin (Rifadin, Rimactane), Ethambutol (Myambutol) na Pyrazinamide.

Kuhakikisha matibabu kamili, mara nyingi inapendekezwa kuwa mgonjwa ameze vidonge mbele ya mtu atakayesimamia matibabu. Njia hii inajulikana kuwa DOTS (matibabu yanayofuatiliwa moja kwa moja, muda mfupi). DOTS hutibu kifua kikuu kwa 95% ya wagonjwa.
Previous
Next Post »